Friday, April 2, 2010

Vodacom yatoa msaada wa kompyuta 20 meatu secondary

Kampuni ya Simu za mkononi ya Vodacom- imetoa msaada wa kompyuta 20 kwa shule mbili za sekondari za Samuye na Meatu mkoani Shinyanga .

�Mkuu wa kanda ya ziwa wa kampuni hiyo Bwana Stephen Kingu ameseme msaada huo umetolewa na kampuni yake kupitia kitengo chake cha misaada kwa jamii.

Amesema lengo ni kuwawezesha wanafunzi wa shule hizo kujifunza masomo ya kompyuta ili wawe na uwelewa mpana wa teknolojia ya habari na mawasiliano.

Naye Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Kanali Mstaafu Edmund Mjengwa amewataka wanafunzi wa kike wa shule za sekondari mkoani humo kujiepusha na upokeaji wa zawadi ndogo ndogo zenye ushawishi kutoka kwa wanaume kwa lengo la kuwataka kimapenzi.
  • SOURCE: Radio One

No comments:

Post a Comment