Friday, April 30, 2010

CHINYULI,EMMANUEL AND AVIT BENEDICTO ON PHOTO

MATOKEO KIDATO CHA SITA: Shule za Serikali zaibuka kidedea

Boniface Meena

SHULE za sekondari za serikali zimeng'ara katika matokeo ya kidato cha sita baada ya wanafunzi wake tisa kuwa miongoni mwa wanafunzi kumi bora kitaifa.Lakini shule hizo za serikali hazikuweza kufua dafu kwa upande wa wasichana baada ya shule binafsi kutoa wanafunzi nane kati ya kumi bora waliofanya vizuri kwenye mtihani huo wa kumaliza elimu ya juu ya sekondari.

Wanafunzi wote walioshika nafasi kumi za kwanza ni wavulana. Wanafunzi hao ni Japhet John wa Shule ya Sekondari ya Ilboru, Manyanda Chitimbo (Kibaha, Pwani), Hassan Rajab (Minaki, Pwani), Abdulah Taher, Stinin Elias, Paul Nolasco na Ephraim Swilla wote kutoka Mzumbe, Morogoro.

Wengine ni Alexander Marwa na Benedicto Nyato kutoka Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Tabora, wakati Samuel Killewo wa Shule ya Sekondari ya Feza Boys ndiye mwanafunzi pekee kutoka shule binafsi aliyeingia kumi bora.

Kwa upande wa shule za wasichana, Jacqueline Seni wa Shule ya Sekondari ya Marian Girls iliyo Bagamoyo mkoani Pwani ndiye aliyeongoza akiwa na wenzake Khadija Mahanga, Esther Mlingwa, Perpetua Lawi na Lilian Kakoko, wakati Gerida John na Subira Omary wanatoka Shule ya Sekondari Dakawa.

Wasichana wengine waliofanya vizuri ni Elaine Kinoti kutoka Ashira, Kilimanjaro, Ruth Pendaeli kutoka Shule ya Sekondari ya Morogoro na Cecilia Ngaiza kutoka St Joseph Ngarenaro, Arusha Cecilia.

Shule za Marian Girls, Mzumbe, Kibaha, Tabora Boys, Ilboru, Malangali, Kifungilo, Tukuyu, Feza Boys na Uru Seminary zimeingia katika kumi bora wakati shule ya High-View International, Fidel Castro, Sunni Madressa, Neema Trust, Mtwara Technical, Muheza, Tarakea, Uweleni, Arusha Mordern na Maswa Girls zimekuwa shule kumi zilizoshika mkia.

Jumla ya watahiniwa 55,764, ambao ni asilimia 88.86 ya wanafunzi wote waliofanya mtihani huo mwaka huu, wamefaulu na kati ya hao wasichana waliofaulu ni 21,821 (sawa na asilimia 90.39) ya waliofanya mtihani na wavulana waliofaulu ni 33,943 (sawa na asilimia 87.90 ya wavulana waliofanya mtihani).

Kwa kulinganisha na mwaka jana wakati waliofaulu walikuwa wanafunzi 45,217 (sawa na asilimia 89.64), idadi ya watahiniwa waliofaulu imeongezeka kwa wanafunzi 10,048, hata hivyo asilimia ya ufaulu imepungua kidogo kwa asilimia 0.78 mwaka huu.

Akitangaza matokeo hayo jana jijini Dar es Salaam, katibu mtendaji wa Baraza la Mitihani(Necta), Dk Joyce Ndalichako alisema watahiniwa wa shule waliofaulu ni 45,217 sawa na asilimia 93.76 ya waliofanya mtihani; wasichana waliofaulu ni 17,905 sawa na asilimia 94.07 na wavulana ni 27,320 sawa na asilimia 93.56.

“Ukilinganisha idadi hiyo na mwaka jana ambapo watahiniwa 36,472 sawa na asilimia 94.37 ya watahiniwa wa shule waliofaulu, idadi ya waliofaulu imeongezeka mwaka huu kwa wanafunzi 8,745 wakati asilimia ya ufaulu imeshuka kidogo kwa asilimia 0.61,” alisema Dk Ndalichako.

Kwa watahiniwa wa kujitegemea, Dk Ndalichako alisema waliofaulu mtihani ni 10,547 sawa na asilimia 72.57 ya wote na kwamba ikilinganishwa na mwaka jana watahiniwa 9,244 sawa na asilimia 74.84 walifaulu, hali inayoonyesha kuwa idadi ya waliofaulu imeongezeka kwa watahiniwa 1,303.

Dk Ndalichako alisema kuwa ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja waliyopata watahiniwa wa shule unaonyesha kuwa jumla ya watahiniwa 39,625 (sawa na asilimia 82.17) wamefaulu kati daraja la kwanza hadi la tatu, wakiwemo wasichana 15,650 (sawa na asilimia 82.22) na wavulana 23,975 (asilimia 82.13).

“Hata hivyo Necta imesitisha kutoa matokeo ya kwa watahiniwa 484 ambao hawajalipa ada ya mtihani na matokeo yao yatatolewa mara watakapolipa ada,” alisema.

Pia imesitisha matokeo ya watahiniwa 49 waliofanya mtihani huku wakiwa na sifa zenye utata matokeo yao yatatolewa mara watakapowasilisha vyeti vyao halisi vya kidato cha nne kwa ajili ya uhakiki pamoja na vielelezo vya kuthibitisha uhalali wao.

Mbali na kufuta matokeo hayo, Necta luimefuta matokeo ya mwaka 2009 kwa watahiniwa 31 wa shule na watahiniwa 105 wa kujitegemea waliobainika kufanya udanganyifu katika mtihani huo.

“Mwaka 2009 watahiniwa nane wa shule na watahiniwa 17 wa kujitegemea walibainika kufanya udanganyifu na matokeo yao yote yalifutwa,” alisema Dk Ndalichako.

Alisema kuwa watahiniwa watatu pia wamefutiwa matokeo yao baada ya kufanya mtihani bila kuwa na sifa zinazostahili ikiwa ni pamoja na kughushi vyeti au kutumia sifa za watu wengine.

Akizungumza na Mwananchi, Jackline Seni, ambaye aliongoza kwa upande wa wasichana, alisema anamshukuru Mungu kwa yote na kwamba sasa ana uhakika wa atasoma Chuo kikuu chochote kile duniani.

Seni, ambaye anaishi Kijitonyama jijini Dar es salaam, alisema kuwa haamini kilichotokea lakini anamshukuru Mungu kwa yote.

“Yani we acha tu sikutegemea hivi, lakini nimeonyesha kuwa wanawake tunaweza,” alisema Jackline ambaye alikuwa akichukua masomo ya uchumi, jiografia na hesabu (EGM).

Alisema kuwa matokeo hayo yamempa faraja kwa kuwa hata katika matokeo ya kidato cha nne ya mwaka 2007 alikuwa wa nne kitaifa na aliongoza katika somo la hesabu na fizikia.

Alisema alipenda kuwemo katika kumi bora ya jumla kwa kuwashinda wavulana, lakini alichokipata kinamtosha kwa kuwa ana uhakika wa kusoma chuo kikuu chochote hapa nchini na nje ya nchi.

“Ninachoomba ni niweze kufanya vizuri huko chuoni na kumaliza vyema kama ilivyokuwa huko nyuma... naamini wasichana na wanawake kwa ujumla tunaweza na tutafika mbali,” alisema Jackline Seni ambaye aliwakumbuka wenzake wa Shule ya Mirian Girls na kuwataka wafanye vizuri zaidi na kuitangaza shule hiyo.

Thursday, April 29, 2010

Mwenyekiti aliyeamuru walimu wachapwe mbaroni

na Stella Ibengwe, Meatu



JESHI la Polisi wilayani Meatu, mkoani Shinyanga linamshikilia Mwenyekiti ya Mtaa wa Kisesa, Ibrahimu Karango (CUF) kwa tuhuma za kuitisha mkutano wa hadhara uliosababisha walimu watatu kuchapwa viboko na sungusungu wa Kata ya Sakasaka.

Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Abiudi Saidea, alisema mbali ya kufikishwa katika vyombo vya sheria, mwenyekiti huyo pia wilaya imelazimika kuvunja uongozi wa sungusungu katika kata hiyo.

Mkuu huyo wa wilaya alisema sungusungu wako kisheria na waliwekwa kisheria isipokuwa wamefanya makosa kujichukulia sheria mkononi na kuongeza kuwa kwa sasa hakuna viongozi wa sungusungu katika kata hiyo hadi pale wilaya inakapokaa na kuamua nani awe kiongozi kwa kufuata taratibu zilizopo.

Alisema hizo ni hatua za awali za kuchunguza ikiwa ni pamoja na kuwachukulia hatua wale wote waliohusika katika zoezi hilo la kuwatandika viboko walimu, ambapo chanzo chake kwa kina kinachunguzwa na vyombo vya usalama.

Hata hivyo Saidea aliwataka wananchi wa Wilaya ya Meatu kuwa watulivu katika kipindi hiki ambacho wanachunguza tukio hilo ambalo limeweka wilaya katika sura ya kipekee kuanzia ngazi ya mkoa hadi taifa.

Mkuu huyo wa wilaya amewaasa wanafunzi wa shule hiyo kuendelea kuwatii walimu pamoja na kufuata sheria zote za shule na si kuchukulia suala la walimu wao kutandikwa viboko kama ni njia ya kuwadharau katika utendaji wao wa kazi.

Tukio la kutandikwa viboko walimu hao lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo walimu watatu wa Shule ya Kisesa walitandikwa kwa kile kinachodaiwa kuwa walichelewa kufika katika mkutano wa sungusungu ndipo mwenyekiti wa mtaa huo alipoamua kuamrisha sungusungu kuwacharaza viboko walimu.

Tukio kama hilo la walimu kuchapwa viboko lilishawahi kutokea katika Mkoa wa Kagera ambapo walimu walicharazwa fimbo na mkuu wa wilaya.

Sungusungu wawavua nguo walimu na kuwachapa viboko

Walimu watatu wa kike na mke mmoja wa mwalimu wa kijiji cha Sakasaka, tarafa ya Kisesa wilayani Meatu, wamevuliwa nguo na kucharazwa viboko na walinzi wa jadi sungusungu wa kijiji hicho kwa madai ya kutohudhuria mkutano uliokuwa umeitishwa na jeshi hilo.

Imedaiwa kuwa walimu hao walishindwa kwenda kwenye mkutano huo kwa sababu ni wajawazito jambo ambalo sungusungu hao walipinga na kuwalazimisha wavue nguo kuthibitisha kama kweli ni wajawazito mbele ya mkutano huo.

Tukio hilo la aina yake na udhalilishaji kijinsia, lilitokea AprilI 7, mwaka huu kati ya saa na 4:00 na 5:00 asubuhi kijijini hapo.

Katibu wa Chama cha Walimu (CWT) wa wilaya ya Meatu, Baraka Owawa, aliiambia Nipashe kuwa walimu hao walikamatwa na sungusungu hao na kuanza kuwapiga, kuwavua nguo kwa madai ya kutohudhuria mkutano.

Owawa alisema walimu hao hawakuwa na jinsi yoyote ya kukabiliana na sungusungu hao bali walitii amri hiyo ya askari hao wa jadi kunusuru maisha yao.

Mara baada ya walimu hao kufanyiwa unyama huo, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Julius Mtuli, alitoa taarifa kwa uongozi wa juu wilayani hapa ikiwemo polisi na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Meatu na timu maalum kuundwa kwenda kijijini hapo kufuatilia suala hilo.

Katika kufuatilia tukio hilo, juzi timu hiyo iliyojumuisha maafisa kutoka ofisi ya Mkuu wa wilaya, Afisa Elimu wa Wilaya, Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSD) Mkaguzi Mkuu wa Shule za Msingi hadi kijijini hapo na polisi kukutana na uongozi wa kijiji hicho.

Katika kikao cha pamoja na uongozi wa serikali ya kijiji, ulikiri kutokea kwa tukio hilo lakini ulisita kuwataja wahusika wa tukio hilo kwa kile kinachodaiwa ni kuogopa fitina kijijini hapo.

Aidha, uongozi huo uliomba radhi kwa walimu wote kwa niaba ya sungusungu waliofanya kitendo hicho ambalo walimu wamelilaani.

Pamoja na uongozi huo kusita, polisi wametoa amri ya uongozi wa kijiji hicho akiwemo Mwenyekiti wa serikali ya kijiji, Afisa Mtendaji wa kijiji, Kamanda na Katibu Mkuu wa Sungusungu kufika kituo kikuu cha polisi cha mjini Mwanhuzi Aprili 19, mwaka huu wakiwa na taarifa kamili na majina ya wahusika waliosababisha udhalilishaji huo kwa walimu.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Mtuli alisema walimu katika kijiji hicho chenye shule mbili za msingi za Sakasaka `A' na `B', wamekilaani kitendo hicho na wamekatishwa tamaa na tabia hiyo na kuomba CWT iwasaidie kumwomba mwajiri wao wahamishwe kijijini hapo.

Mwalimu huyo wa Shule ya Msingi Sakasaka `B' aliongeza kuwa wananchi wa kijiji hicho wamekuwa na tabia ya kuwadhalilisha walimu na wafanyakazi wengine wanaofanyakazi eneo hilo ikiwemo kuwapiga, kuwatishia maisha, kuwanyanyasa na kutothaminiwa.

Mei, mwaka jana, mwalimu mmoja wa kiume (jina limehifadhiwa), pia alipigwa na kuvuliwa nguo zake alizovaa na kumwacha kama alivyozaliwa.

Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Abiud Saideya, alipozungumza na Nipashe kwa njia simu alikiri kutokea kwa tukio na tayari ametoa maelekezo kwa maafisa wake na kuahidi kutoa maelezo zaidi kwa kuwa yuko nje ya wilaya yake kikazi.

Sungusungu wawavua nguo walimu na kuwachapa viboko

Walimu watatu wa kike na mke mmoja wa mwalimu wa kijiji cha Sakasaka, tarafa ya Kisesa wilayani Meatu, wamevuliwa nguo na kucharazwa viboko na walinzi wa jadi sungusungu wa kijiji hicho kwa madai ya kutohudhuria mkutano uliokuwa umeitishwa na jeshi hilo.

Imedaiwa kuwa walimu hao walishindwa kwenda kwenye mkutano huo kwa sababu ni wajawazito jambo ambalo sungusungu hao walipinga na kuwalazimisha wavue nguo kuthibitisha kama kweli ni wajawazito mbele ya mkutano huo.

Tukio hilo la aina yake na udhalilishaji kijinsia, lilitokea AprilI 7, mwaka huu kati ya saa na 4:00 na 5:00 asubuhi kijijini hapo.

Katibu wa Chama cha Walimu (CWT) wa wilaya ya Meatu, Baraka Owawa, aliiambia Nipashe kuwa walimu hao walikamatwa na sungusungu hao na kuanza kuwapiga, kuwavua nguo kwa madai ya kutohudhuria mkutano.

Owawa alisema walimu hao hawakuwa na jinsi yoyote ya kukabiliana na sungusungu hao bali walitii amri hiyo ya askari hao wa jadi kunusuru maisha yao.

Mara baada ya walimu hao kufanyiwa unyama huo, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Julius Mtuli, alitoa taarifa kwa uongozi wa juu wilayani hapa ikiwemo polisi na ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Meatu na timu maalum kuundwa kwenda kijijini hapo kufuatilia suala hilo.

Katika kufuatilia tukio hilo, juzi timu hiyo iliyojumuisha maafisa kutoka ofisi ya Mkuu wa wilaya, Afisa Elimu wa Wilaya, Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSD) Mkaguzi Mkuu wa Shule za Msingi hadi kijijini hapo na polisi kukutana na uongozi wa kijiji hicho.

Katika kikao cha pamoja na uongozi wa serikali ya kijiji, ulikiri kutokea kwa tukio hilo lakini ulisita kuwataja wahusika wa tukio hilo kwa kile kinachodaiwa ni kuogopa fitina kijijini hapo.

Aidha, uongozi huo uliomba radhi kwa walimu wote kwa niaba ya sungusungu waliofanya kitendo hicho ambalo walimu wamelilaani.

Pamoja na uongozi huo kusita, polisi wametoa amri ya uongozi wa kijiji hicho akiwemo Mwenyekiti wa serikali ya kijiji, Afisa Mtendaji wa kijiji, Kamanda na Katibu Mkuu wa Sungusungu kufika kituo kikuu cha polisi cha mjini Mwanhuzi Aprili 19, mwaka huu wakiwa na taarifa kamili na majina ya wahusika waliosababisha udhalilishaji huo kwa walimu.

Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Mtuli alisema walimu katika kijiji hicho chenye shule mbili za msingi za Sakasaka `A' na `B', wamekilaani kitendo hicho na wamekatishwa tamaa na tabia hiyo na kuomba CWT iwasaidie kumwomba mwajiri wao wahamishwe kijijini hapo.

Mwalimu huyo wa Shule ya Msingi Sakasaka `B' aliongeza kuwa wananchi wa kijiji hicho wamekuwa na tabia ya kuwadhalilisha walimu na wafanyakazi wengine wanaofanyakazi eneo hilo ikiwemo kuwapiga, kuwatishia maisha, kuwanyanyasa na kutothaminiwa.

Mei, mwaka jana, mwalimu mmoja wa kiume (jina limehifadhiwa), pia alipigwa na kuvuliwa nguo zake alizovaa na kumwacha kama alivyozaliwa.

Mkuu wa Wilaya ya Meatu, Abiud Saideya, alipozungumza na Nipashe kwa njia simu alikiri kutokea kwa tukio na tayari ametoa maelekezo kwa maafisa wake na kuahidi kutoa maelezo zaidi kwa kuwa yuko nje ya wilaya yake kikazi.

Thursday, April 22, 2010

: Hakuna mwalimu anayeidai serikali

SERIKALI imesema hadi sasa hakuna mwalimu yeyote anayedai mshahara wala posho ya kujikimu kwa mwaka 2009/2010, Bunge limeelezwa.

Tamko hilo lilitolewa bungeni jana na Naibu Waziri (TAMISEMI), Agrey Mwanri, alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Mufindi Kusini, Benito Malangalila (CCM).

Katika swali hilo, Malangalila alitaka kujua ni sababu zipi zinazofanya mishahara ya walimu kucheleweshwa, hatua inayosababisha kero na usumbufu mkubwa hasa kwa walimu wapya wanaoajiriwa.

Akijibu swali hilo, Mwanri alisema baada ya serikali kuanzisha utaratibu mpya ulioanza kutumika Septemba, 2009 mishahara ya walimu wapya inafikishwa vituoni katika mwezi husika ambao mwalimu anapangiwa.

“Aidha wizara yangu imeziagiza halmashauri zote nchini kuwalipa walimu posho ya kujikimu ya siku saba mara tu mwalimu anapofika kuanza kazi. Zoezi hili limefanyika kwa mafanikio makubwa,” alisema.

Tuesday, April 13, 2010

Bibi kizee amchangia Kikwete 200/-

BIBI Milembe Ndugulile (81), ambaye ni mkazi wa mkoa wa Shinyanga vijijini, ametoa mchango wa sh 200 ukiwa ni mchango wake kwa Rais Jakaya Kikwete ili kumwezesha kununua fomu ya kuwania tena urais endapo ataamua kufanya hivyo.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Idara ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Ikulu, imeeleza kuwa bibi huyo, ametoa mchango wake huo wa sarafu moja ya sh 200 katika mchango wa jumla wa wananchi wa Shinyanga wa kumwunga mkono Rais Kikwete katika kinyang’anyiro cha kuwania kiti hicho katika uchaguzi mkuu ujao.

Mchango huo ulikuwa miongoni mwa sh 1, 482,200, ambazo alikabidhiwa Rais Kikwete na Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga, Hamisi Mgeja, katika halfa fupi iliyofanyika Ikulu Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Katika risala iliyosomwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) wa Mkoa wa Shinyanga, Stepehen Masele, kabla ya Ngeja kukabidhi fedha hizo, ilielezwa kuwa fedha hizo zilitokana na michango ya hiari ya papo kwa hapo ya wananchi wa Shinyanga, wakati wa tafrija ya kuwasimika makamanda wapya wa UVCCM wa mkoa huo, iliyofanyika Machi 3, mwaka huu, mjini Shinyanga.

Mwenyekiti huyo wa mkoa alimweleza Rais Kikwete kuwa Bibi Milembe Ndugulile alikuwa amesisitiza kuwa fedha hizo (sarafu moja ya sh 200) zifikishwe kwa Rais Kikwete, kama mchango wake binafsi kuonyesha furaha yake kwa uongozi wake katika miaka minne iliyopita.

“Bibi Ndugulile ameniagiza nikuambie kuwa sh 200 ndiyo uwezo wake na ni fedha ndogo, lakini ni ishara ya kuonyesha dhamira yake kuwa ataendelea kuunga mkono uongozi wako kutokana na mengi ambayo umeifanyia nchi hii katika miaka minne iliyopita katika kulinda utaifa, umoja, mshikamano, amani na utulivu,” alieleza Ngeja.

Akitoa shukurani zake, Rais Kikwete, alisema ameupokea kwa dhati mchango huo wa Bibi Ndugulile na kwamba ni muhimu sana kwake.

“Mchango huu ni muhimu sana kwangu, ni mchango unaoonyesha upendo wa bibi huyo kwangu na utanisaidia kuifanya hiyo kazi, baada ya uamuzi kuwa umechukuliwa kuhusu suala hili.”

Sunday, April 11, 2010

Raundi ya pili Liyumba kidedea

Happiness Katabazi



MEI, 31 mwaka jana niliandika makala katika gazeti hili iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho: “Raundi ya kwanza Liyumba kidedea.” Paragrafu ya kwanza ilikuwa na maneno yasemayo, ‘Vita dhidi ya ufisadi vilianza kwa kishindo. Kwa kishindo hichohicho itamalizika bila ya wananchi kujua imemalizika kwa namna gani.”

Nilifikia uamuzi wa kuandika makala hiyo baada ya Hakimu Mkazi, Waliarwande Lema, Mei 27 kuifuta kesi ya matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali hasara ya sh bilioni 221 iliyokuwa ikimkabili aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu, Amatus Liyumba, na meneja mradi majengo ya minara pacha katika benki hiyo, Deogratius Kweka.

Hakimu huyo aliifuta kesi hiyo baada ya upande wa mashtaka uliokuwa ukiongozwa na Wakili Kiongozi Justus Mulokozi kukiri mbele ya mahakama hiyo kuwa hati ya mashtaka ilikuwa imekosewa lakini muda mfupi baada ya washtakiwa kuachiliwa walikamatwa tena.

Mei 28 mwaka jana, Liyumba anayetetewa na mawakili wa kujitegemea Jaji Mstaafu Hillary Mkate, Majura Magafu, Onesmo Kyauke na Hudson Ndusyepo peke yake ndiye aliyerudishwa mahakamani hapo na kufunguliwa kesi mpya ya jinai Na.105/2009 ambapo mashitaka yalikuwa ni yale yale ya matumuzi mabaya na kusababisha hasara ya sh bilioni 221, huku Kweka akiachwa huru.

Tangu kipindi hicho hadi sasa Liyumba ameendelea kusota rumande kwa sababu ameshindwa kutimiza masharti ya dhamana yaliyomtaka atoe fedha taslimu au kuwasilisha hati ya mali yenye thamini ya sh bilioni 110.

Aidha, Septemba 20 mwaka jana, katika gazeti hili niliandika makala iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho, “Watanzania wategemee nini kwenye ‘PH’ ya Liyumba?”

Ndani ya makala hiyo nilimweleza DPP kwamba kama mkoba wake katika kesi hiyo haukuwa na ushahidi madhubuti ni vizuri angeiondoa mapema mahakamani ili wasipoteze muda wa mahakama na fedha za walipa kodi.

Baada kuandika makala hizo baadhi ya wanasheria wa serikali waandamizi walinipongeza kwa makala hizo kwani zina ukweli mtupu na wakaniuma sikio na kunieleza mwisho wa siku serikali itashindwa kufurukuta katika kesi hiyo na walidiriki kuifananisha kesi hiyo na ‘sinema’.

Nimewahi kuandika kuwa Sheria ya Taasisi ya Kuzia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ya mwaka 2006 ilitungwa kwa shinikizo la wafadhili, serikali iliburuzwa miguu kwa miaka kadhaa lakini hatimaye ilisalimu amri pale wafadhili walipotishia kuwa wasingetoa mikopo, misaada katika nchi ambazo zisingeonyesha nia ya kupambana na rushwa (ufisadi sasa), dawa za kulevya na ugaidi.

Tanzania ilisalimu amri haraka na ikatunga sheria ya ugaidi ambayo ni kinyume kabisa na haki za binadamu na ikatunga sheria ya rushwa iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2006 ambayo inatumika hivi sasa. Kwa hiyo tunaona serikali yetu haikuwa na nia ya dhati ya kupambana na majanga hayo, ila sheria hizo zilitungwa kishabiki, kishikaji na kisanii.

Nimelazimika kutumia kumbukumbu hizo sahihi hapo juu ili ziweze kuunga mkono mada yangu ya leo ambayo nitajadili uamuzi uliotolewa April 9 mwaka huu na Kiongozi wa Mahakimu Wakazi (Edson Mkasimongwa), Lameck Mlacha na Benedict Mwingwa wa kumfutia shitaka moja kati ya mashitaka mawili yaliyokuwa yakimkabili Liyumba.

Kwa maelezo kuwa upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha kupeleka ushahidi wa kuthibitisha shitaka la pili ambalo ni la kuisababishia serikali hasara. Aidha imemuona Liyumba ana kesi ya kujibu katika shitaka la kwanza la matumizi mabaya ya ofisi ya umma.

“Mahakama inaamini alichokizungumza Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Juma Reli, katika ushahidi wake ni ukweli mtupu na ndiyo maana alivyomaliza kutoa ushahidi wake alitoka ndani ya mahakama hii kwa amani na mawakili wa serikali hawakulalamika kwamba shahidi wao ametoa ushahidi wa uongo…kwa hiyo mahakama hii inatamka kiasi cha fedha kilichoongezeka katika ujenzi wa mradi ule kilitumika kwa utaratibu wa fedha za serikali zinavyotakiwa zitumike.

“Kwa heshima na taadhima jopo hili halikubaliani na hoja ya upande wa mashitaka iliyotaka mahakama hiyo isikubaliane na hoja ya upande wa utetezi iliyosema huwezi kuthibitisha hasara katika mradi huo hadi uwe na ripoti ya mwisho ya fedha zilizotumika kwenye mradi ule kwa sababu hata ripoti hiyo ingekuwepo isingeweza kuondoa makadirio ya gharama zilizokadiriwa na mkadiriaji wa majengo wa mradi huo.

“Mahakama inasisitiza haikubaliani na hoja hiyo ya upande wa mashitaka kwa sababu katika kesi hiyo hasara iliyodaiwa amepata mwajiri wa mshitakiwa ni lazima ithibitishwe kwa namba na ripoti…sasa katika kesi hii hasara iliyopatikana haiwezi kuwa sawa na namba ya ripoti ya Mkadiriaji wa Majengo kwani majengo ya nyongeza yamejengwa …labda ingekuwa majengo hayo mengine yanayodaiwa kujengwa nje ya mkataba wa awali na fedha hazionekana hilo lingekuwa ni jambo jingine.

“Na upande wa mashitaka wenyewe kupitia mawakili wake ukiri mbele yetu kwamba makadirio ya awali yaliyapaswa kujengwa magorofa 14 lakini baada ya mabadiliko ya ongezeko la ujenzi ziliongezeka ghorofa tatu nyingine juu hivyo kufanya kuwa na majengo mawili na kila jengo lina ghorofa 17 kwenda juu na kweli majengo yamejengwa …

“Kwa maelezo hayo mahakama hii inamfutia mshitakiwa shitaka la pili kwa mujibu wa kifungu cha 230 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ya mwaka 2002 an na akaueleza upande wa mashitaka upo huru kukata rufaa kama haujalidhika na uamuzi huo,” alisema Mkasimongwa na kusababisha ndugu na jamaa wa mshitakiwa wakisikika kwa sauti wakisema, ‘Asante Yesu.’

Kutokana na uamuzi huo wa Hakimu Mkazi Mkasimongwa na wanajopo wenzake, umedhihirisha pasipo shaka kwamba wachunguzi wa TAKUKURU ambao ndiyo walipeleleza kesi hii, na waendesha mashitaka walikuwa hawajui walichokuwa wanakifanya katika kuthibitisha shitaka hilo lililofutwa au walikuwa wakijua ila waliamua kumuandalia kumshitaki Liyumba.

kwa shitaka hilo makusudi mazima ili wamkomeshe kwasababu walijua hawezi kutimiza masharti na hivyo ni lazima angesota jela kwa sababu kisheria mahakama inapotoa masharti ya dhamana kwa mshitakiwa wa kesi yoyote ile ni lazima masharti hayo yatimizwe na si vinginevyo na endapo mshitakiwa anashindwa kutumiza anatakiwa aende rumande hadi atakapoyatimiza masharti husika.

Kama mawakili wa serikali ambao tunawashuhudia wakija pale mahakamani kwa mikogo huku wakiwa wanayaburuza masanduku kama wamehifadhi nyoka kwenye masanduku hayo na kuvalia suti utadhani ni wachungaji waliokimbiwa na waumini’ kama hawana taaluma ya kutosha kwa nini wasiombe ushirikiano wa kitaalum toka kwa mawakili wengine wenye ujuzi ambao mawakili wengine binafsi walikuwa walimu wenu vyuoni?

Serikali sasa iache uchoyo na ukiritimba katika mambo ya kitaaluma, ipende kushirika wanataluuma wenye uwezo kwenye maeno yao. Naomba kutoa hoja.

Nayasema haya kwa uchungu kwasababu ni kodi za wanachi ndizo zilizowasomesha mawakili wengi wa serikali na ndizo zinazotumika kuwalipa mishahara na fedha hizo za wavuja jasho zinazotumika kuwaweka hotelini baadhi ya mawakili wanakwenda kujichimbia katika hoteli hizo kuandika hoja mbalimbali katika kesi zilizofunguliwa na jamhuri.

Kama hawa mawakili wa serikali wanapokea mishahara inayotokana na kodi zetu, wananchi tuna haki ya kuhoji mambo wanayoyafanya ambayo hayaturidhishi.

Baadhi ya mawakili wetu wa serikali wanaonekana kuwa dhaifu na wababaishaji katika kesi wanazozisimamia na wakati mwingine nimekuwa kijiuliza akilini mwangu ubabaishaji huo unatokana ama wakati wapo vyuoni walikuwa wakiangalizia majibu kutoka kwa wenzao au walikuwa wakiiba mitihani.

Sasa kubabaikababaika kwa mawakili wa serikali waliokuwa wakiongozwa na Juma Mzarau aliyekuwa akisaidiwa na Prosper Mwangamila na Ben Lincolin katika kesi ya Liyumba hadi kusababisha mahakama hiyo awali kumfutia kesi mshitakiwa kwa sababu hati ya mashitaka ilikuwa imekosewa na juzi Hakimu Mkazi Mkasimongwa kumfutia shitaka moja mshitakiwa kwasababu upande wa mashitaka umeshindwa kuthibitisha shitaka hilo la kusababisha hasara ni dhahiri ni ishara mbaya kwa shitaka lilobaki.

La matumizi mabaya, Watanzania sasa tujiulize kama jamhuri imeshindwa kuthibitisha shitaka la kusababisha hasara ambapo shitaka hilo linakuja baada ya mtu kutumia ofisi yake vibaya. Je upande wa mashitaka wanauakikishiaje umma kwamba mwisho wa siku wataweza kuthibitisha shitaka la matumuzi mabaya? Hilo tuliachie mahakama kwani mwisho wa siku itatoa hukumu yake kutokana shitaka hilo, ni suala la muda, tusubiri tuone.

Je, itakapotekea watuhumiwa wa kuachiwa huru si kesi zitakuwa zimekwisha kwa kishindo kile kile kama zilivyofunguliwa kwa kishindo? Tuseme nini sasa.usanii mtupu au ufisadi mtupu unaofanywa na mawakili wetu wa serikali?

Kushindwa kufurukuta kwa serikali katika shitaka hilo, nawaomba wananchi wenzangu wawe pamoja na sisi waandishi wa habari za mahakama kufuatilia kesi kama hizi zilizosalia mahakamani mfano kesi ya matumuzi mabaya na kuisababishia serikali hasara ya sh bilioni 11 inayomkabili aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba,Gray Mgonja na Daniel Yona; kesi nyingine ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia Profesa Costa Mahalu na Mkurugenzi Fedha na Utawala wa ubalozi huo Grace Martin ili hatimaye tukoleze kiu ya Watanzania katika harakati za kupambana na ufisadi.

Mwisho kabisa naupongeza Mhimili wa Mahakama nchini kwa kujipambanua kama chombo cha kutoa haki bila upendeleo, kushinikizwa na bila kuogopa. Jopo la mahakimu wakazi linalosikiliza kesi hiyo, Mkasimongwa, Mlacha na Mwingwa kutokana na uamuzi wake juzi nadiriki kusema kuwa limefanya kazi ya kishujaa na iliyoendelea kuuletea heshima mhimili wa mahakama wa nchi yetu.

Sisi tuliokuwa tunahudhuria kesi hii tangu ilipofunguliwa mahakamani hapo Januari 26 mwaka jana hadi juzi, tumeshuhudia vituko, shinikizo, ubabe uliojidhihirisha kwa wingi wa makachero waliokuwa wanaipamba mahakama ya Kisutu kwa staili tofauti kila kukicha.

Thursday, April 8, 2010

TAMKO LA CHAMA CHA WAAJIRI TANZANIA (ATE) KUHUSU NOTISI YA MGOMO WA WAFANYAKAZI WOTE ILIYOTOLEWA NA SHIRIKISHO LA VYAMA VYA WAFANYAKAZI TANZANIA TUCTA

Chama cha Waajiri Tanzania kimepokea kwa mshangao mkubwa notisi ya mgomo usio na ukomo unaohusu wafanyakazi wote wa sekta za umma na binafsi.

Sisi tunashangaa kwa sababu tunaamini katika majadiliano baina ya vyama vya wafanyakazi na waajiri ikiwemo serikali kama njia bora ya kuendeleza tija sehemu za kazi na hali bora za wafanyakazi. Ni katika majadiliano tofauti za kimsingi hupatiwa suluhu. Ni pale tu ama mazingira ya majadiliano hayapo au majadiliano yenyewe yamekwama ndipo hapo silaha ya mwisho ya wafanyakazi ambayo ni mgomo hutumika.

Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) kimechunguza kwa makini sababu saba (7) zilizotolewa katika notisi iliyotolewa na Shirikisho la Vyama Vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) na tumeridhika mazingira ya kutangaza mgomo hayapo kwa sasa.

Sababu saba zilizotolewa na TUCTA ni:-

1. Kutotekeleza mapendekezo ya Tume ya Mishahara ya NTUKAMAZINA ambayo iliteuliwa na Mheshimiwa Rais kuboresha maslahi ya wafanyakazi.

TUCTA haijaweka bayana Tume ya Mishahara ya NTUKAMAZINA ilipendekeza nini. Tujuavyo sisi ripoti husika ilikuwa ni ya siri na ilikuwa kwa matumizi ya Mhe. Rais aliyeiteua. Isitoshe TUCTA inaelekea inataka kumlazimisha Rais atekeleze mapendekezo ya Tume yasiyoainishwa. Tunaamini huku ni kwenda kinyume na Katiba ya Nchi kwa kuingilia madaraka ya Rais.

2. Kutoliangalia suala zima la ukusanyaji wa kodi, hivyo kuwafanya wafanyakazi kuwa eneo kubwa pekee la kulipa kodi za juu wakati wafanyabiashara wakilipa kodi ndogo na wakati mwingine kukwepa.

Haiyumkiniki kudai kwamba kodi wanazolipa wafanyakazi ndizo kubwa kulinganisha na maeneo mengine. Idadi ya wafanyakazi katika sekta rasmi ni ndogo na hivyo hawawezi kulipa kodi za kutosheleza mahitaji ya kuendesha nchi. Tunakiri kunaweza kuwepo matatizo katika ukusanyaji wa kodi, lakini hatudhani suluhu ya matatizo haya ni mgomo.

3. Wizara ya Kazi kutotangaza maamuzi yake kuhusu mapendekezo ya utafiti uhusuo Vima vya chini katika sekta binafsi, kinyume na sheria inavyoagiza.

Hakuna sheria inayounda Taasisi ya kutafiti vima vya chini vya mishahara. Taasisi zilizopo ni Bodi za kisekta za mishahara ambazo zina jukumu la kushauri juu ya vima vya chini vya mishahara. Dai la TUCTA hapa ni kuhusu kutangazwa kwa mapendekezo ya Mshauri Mwelekezi ambaye ni Taasisi ya Utafiti wa Uchumi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Economic Research Bureau). Tunachojua ni kwamba taarifa ya utafiti wa Mshauri Mwelekezi pamoja na maoni ya Bodi za Kisekta za mishahara yalijadiliwa katika kikao cha mwisho cha Baraza la Ushauri la Uchumi na Jamii (LESCO) lililokutana tarehe 25 Machi 2010. TUCTA iliwakilishwa katika kikao hiki.

Hivo suala hili limo katika mchakato na hivyo haliwezi kuwa hoja halali ya mgomo. Hata hivyo tunajua Tangazo la Serikali Namba 223 la mwaka 2007 kuhusu vima vya chini vya mishahara bado lina nguvu za kisheria mpaka hapo Mhe. Waziri wa Kazi atakapotangaza vima vipya vya mishahara.

4. Wizara ya Kazi kushindwa kuunda bodi mpya za mishahara za sekta binafsi tangu zile za zamani zilipomaliza muda wake 1 Aprili 2009.

Tunavyofahamu sisi, Bodi za mishahara za kisekta kama vilivyo vyombo vingine vya utatu vinavyoteuliwa chini ya sheria ya Taasisi za Kazi, (Na. 7 ya 2004) vilipewa uhai wa miaka mitatu toka kuundwa kwao. Bodi za mishahara za kisekta ziliundwa Aprili 2007 na hivyo ukomo wake utaishia mwezi huu na si kweli kwamba uhai ulikoma Aprili 2009 kama TUCTA inavyodai. TUCTA inatambua kwamba mchakato wa kuundwa upya kwa Bodi hizi umeanza tangu Machi 2010 na hivyo hii haiwekani kuwa hoja ya kusababisha mgomo.

5. Wizara ya Kazi kushindwa kuitisha vikao vya LESCO ambacho ni chombo cha kuishauri serikali kuhusu masuala ya wafanyakazi tangu chombo hicho kizinduliwe mwezi Agosti 2009 licha ya Raisi kuagiza likutane katika kikao chetu cha 4/5/2009 Ikulu Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa sheria, LESCO inapaswa kukutana angalau mara tatu (3) kwa mwaka. Sheria haijafafanua ni kipindi gani katika mwaka. LESCO iliyopo ilizinduliwa Agosti 2009, inabidi ifikapo Agosti mwaka huu iwe imekutana angalau mara tatu. Mpaka sasa imeshakutana mara mbili na bado tuna miezi minne kufikia Agosti. Hivyo hatuoni utoshelevu wa sababu hii kuhalalisha mgomo.

6. Ofisi ya Waziri anayehusika na Menejimenti ya Utumishi wa Umma kushindwa kuitisha vikao vya majadiliano yanayohusu maslahi ya watumishi wa umma kama sheria ya majadiliano (The Public Service Negotiating Machinery) Act 2003 inavyoagiza.

Hatuoni sababu hii kutosheleza kuita mgomo wa nchi nzima kwa kujumuisha hata wafanyakazi wa sekta binafsi ambao wana utaratibu tofauti wa majadiliano.

7. Serikali kutokuwa makini katika kurekebisha malipo dhaifu yatokanayo na Mifuko ya Pensheni ya Wastaafu hivyo kuwafanya Wastaafu wengi kupata mafao duni ya uzeeni.

Mchakato wa kurekebisha matatizo yaliyopo katika mifuko ya hifadhi ya jamii ulishaanza. Wadau wote katika utatu ikiwemo TUCTA tunafahamu mchakato unaoendelea wa kuunda Mamlaka ya kusimamia mifuko hii (Social Security Regulatory Authority). Kwa kuwa hili ni suala la kimchakato na linalohitaji uangalifu mkubwa, ni maoni yetu kuwa TUCTA imekosa subira inayohitajika kwa jambo muhimu kama hili. Si haki hata kidogo kumlaumu binafsi. Mhe. Waziri wa Kazi. Kwa maana hii hatuoni sababu yeyote ya msingi ya kuitisha mgomo kwa hoja hii.

HITIMISHO

Kutokana na ufafanuzi huu, Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) kinatamka kama ifuatavyo:-

1. Kwamba Notisi iliyotolewa ni wa mgomo usio halali kwa kuwa:-
a) Sababu za mgomo hazipo
b) Njia za majadiliano bado zipo wazi na wala majadiliano hayajashindikana
c) Mgomo uliotangazwa hauna kipindi maalum kinyume na matakwa ya kisheria
d) Mgomo uliotangazwa unahusu sekta zote za uchumi wa nchi ikiwemo sekta binafsi ambayo ina taratibu zake za kuhakikisha na kulinda maslahi ya wafanyakazi.
e) Mgomo huu utahusu pia sekta ya huduma muhimu kwa jamii (essential services) ambazo haziruhusiwi kisheria kugoma.

2. Kwa kuwa mgomo huu si halali, Waajiri watakaoathirika watakuwa na haki ya kuwachukulia hatua za kinidhamu wafanyakazi watakaoshiriki mgomo huu haramu ikiwemo kuwaachisha kazi; kutowalipa mishahara kwa kipindi cha mgomo na hata kuajiri wafanyakazi mbadala. Ijulikane kwa wadau wote kwamba sheria zilizopo hazilindi wafanyakazi wanaoshiriki migomo haramu.

3. Iwapo mgomo huu utatekelezwa, Waajiri watakaoathirika watakuwa na haki ya kudai fidia kwa hasara itakayosababishwa na mgomo dhidi ya TUCTA ilioitisha mgomo usio halali.

4. Waajiri wanayo haki ya kwenda Mahakama Kuu, Kitengo cha Kazi (Labour Division) kuomba nafuu za kisheria.

Tunatoa RAI kwa TUCTA na wadau wote waliohamasishwa na TUCTA, waachane na harakati za kuitisha mgomo ambao utakuwa ni hasara kwa pande zote. Tunainasihi TUCTA washiriki kwa dhati majadiliano yenye lengo la kuleta muafaka wa pamoja. Kwa hili hakuna njia ya mkato. TUCTA itambue kwamba majadiliano baina ya wadau yanajenga hali ya kuaminiana na mahusiano mazuri na endelevu.

Ikumbukwe kwamba amani na utulivu sehemu za kazi ni nguzo muhimu za kuongeza tija, kukuza uchumi, kuwepo kwa ajira endelevu na kupambana na umaskini. Vyama vya Wafanyakazi ni wadau muhimu katika kuendeleza amani na utulivu mahali pa kazi.

Dar es Salaam, 5 Aprili 2010
CHAMA CHA WAAJIRI TANZANIA (ATE)


Wakili Cornelius K. Kariwa
Dkt. Aggrey K. Mlimuka
MWENYEKITI MKURUGENZI MTENDAJI

Tuesday, April 6, 2010

Mrema adai kuna siasa mgomo wa wafanyakazi

MWENYEKITI wa TLP, Augustine Mrema, ambaye amekuwa akitoa kauli zinazoonekana kuitetea serikali ya awamu ya nne, amegeukia mgomo ulioitishwa na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta), akisema una harufu ya kisiasa.

Mrema, ambaye safari hii atagombea ubunge wa jimbo la Vunjo baada ya kushindwa mara tatu katika kinyang'anyiro cha urais, alisema hayo jana jijini Dar es salaam alipokuwa akitoa salamu za siku kuu ya Pasaka za chama hicho.

Mrema, ambaye amekuwa akimsifu Rais Jakaya Kikwete katika miezi ya karibuni, aliitaka Tucta kuheshimu kauli ya rais aliyoitoa katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi Machi mwaka huu, akiwasihi viongozi wa shirikisho hilo kukubali kukaa mezani ili kutafuta suluhu ya matatizo ya wafanyakazi kwa njia ya mazungumzo.

“Utafiti wetu sisi TLP tumegundua kuwa mgomo wa Tucta unatokana na kushinikizwa... una mkono wa kisiasa ndani yake,” alisema Mrema.

Mrema alisema wamegundua kuwa baadhi ya viongozi wanaoshabikia mgomo huo wanatarajia kugombea ubunge katika majimbo yaliyo mikoa ya Kagera na Mara.

“Nasema hivyo kwa sababu kuna taarifa kuwa mgomo huo una msukumo wa viongozi hao kwa masilahi yao binafsi na vyama vyao hivyo ni vyema Tucta ikaheshimu kauli ya Rais ili kuweza kuepuka kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa na viongozi hao kwa kuwahadaa wananchi kuwa wao wana uchungu na wafanyakazi,” alisema.

Alisema Tucta inapaswa kuheshimu kauli hiyo kwa sababu rais alionyesha unyenyekevu mkubwa kwa kuwa alitambua madhara yanayoweza kusababishwa na mgomo.

Mgomo huo, ambao umepangwa kuanza Mei 5, tayari umeshaungwa mkono na vyama mbalimbali vya wafanyakazi, hali inayoashiria kuwa nchi inaweza kusimama iwapo nia hiyo ya kugoma itatekelezwa na Rais Kikwete alizungumzia hilo akisema kuwa maslahi yake kiuchumi yatakuwa makubwa.

“Unyenyekevu aliouonyesha rais wetu ni fundisho hasa kwetu viongozi na unapaswa kuigwa, hivyo mkono wa maridhiano alioutoa unapaswa kupokewa na wafanyakazi wote wenye nia njema,” alisema.

Mrema alisema kutokana na ukakamavu aliouonyesha Rais Kikwete, ni muhimu vyama vya wafanyakazi vikubali kurudi kwenye meza ya mazungumzo bila kumpa rais masharti yoyote.

Katika hatua nyingine Mrema aliwapongeza viongozi wa dini nchini kwa kutoa ujumbe kwa waumini wao unaosisitiza amani, utulivu lakini pia kuwaonya wale wanaohubiri chuki dhidi ya serikali iliyo madarakani.

Mrema alisema viongozi hao wanaohubiri chuki wanapaswa kukumbuka kuwa amani ikitoweka hawatakuwa tena na kondoo wa kuchunga.

Waajiri wawatisha wafanyakazi

Sadick Mtulya

WAKATI Rais Jakaya Kikwete alitumia muda mwingi wa hotuba yake ya kila mwezi kusihi wafanyakazi wakubali kuingia kwenye mazungumzo badala ya kugoma, Chama cha Waajiri Tanzania(ATE) kimeamua kutoa tishio kwa wote ambao watashiriki kwenye mgomo uliopangwa kufanyika kuanzia Mei 5.

Mgomo huo umeitishwa na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta) kwa lengo la kuishinikiza serikali kusikiliza madai yao baada ya kuyapuuza kwa muda mrefu na tayari shirikisho hilo lilishafuata taratibu kwa kutoa notisi ya siku 60 ambazo ziliisha bila ya serikali kuchukua hatua.

Miongoni mwa madai hayo ni kutangazwa kwa kima cha chini cha mishahara, vyombo vilivyoundwa kushughulikia masuala ya wafanyakazi kutofanya kazi na kupanua wigo wa kodi ili kumpunguzia mfanyakazi mzigo, na Rais Kikwete alikiri kuwa mishahara ni midogo na akaahidi kuipandisha.

Lakini ATE ilisema jana kuwa mgomo huo si halali na kuagiza waajiri watakaoathirika na mgomo huo wa nchi nzima, kuwachukulia hatua za kinidhamu wafanyakazi watakaoshiriki, ikiwa ni pamoja na kuwaachisha kazi, kutowalipa mishahara kwa kipindi cha mgomo na hata kuajiri wafanyakazi mbadala.

ATE pia imesema iwapo mgomo huo utatekelezwa, waajiri watakaoathirika watakuwa na haki ya kudai fidia kwa hasara itakayosababishwa na mgomo pamoja na kwenda Mahakama ya Kazi kuomba nafuu za kisheria.

Mkurugenzi mtendaji wa ATE, Dk Aggrey Mlinuka alisema sheria zilizopo hazilindi wafanyakazi wa sekta binafsi wanaoshiriki migomo haramu na kwamba sekta binafsi ina taratibu zake za kuhakikisha na kulinda maslahi ya wafanyakazi.

“Pia, mgomo huu ni haramu kutokana na kwamba kifungu cha sheria namba 85 kilichotumiwa na Tucta hakihusu mgomo usiokuwa na mwisho ila kinahusu protection action (kitendo cha kulinda),” alisema Dk Mlinuka.

“Waajiri watakaoathirika na mgomo huo wawachukulie hatua za kinidhamu wafanyakazi watakaoshiriki mgomo huo ikiwemo kuwaachisha kazi, kutowalipa mishahara kwa kipindi cha mgomo na hata kuajiri wafanyakazi mbadala.”

Awali, mwenyekiti wa ATE, Wakili Cornelius Kariwa alisema wamefika hatua ya kupinga mgomo huo baada ya kuchunguza kwa makini sababu saba zilizotolewa katika notisi iliyotolewa na Tucta kuwa hazijitoshelezi kutangaza mgomo huo.

“Tucta haijaweka bayana Tume ya Mishahara ya Ntukamazina ilipendekeza nini. Tujuavyo sisi ripoti husika ilikuwa ni ya siri na ilikuwa kwa matumizi ya rais aliyeiteua. Isitoshe Tucta inaelekea kumlazimisha rais atekeleze mapendekezo ya Tume yasiyoainishwa.

Tunaamini huku ni kwenda kinyume na katiba ya nchi kwa kuingilia madaraka ya rais,” alisema Kariwa.

Tucta pia inaitaka serikali kuongeza wigo wa walipa kodi ili kuwapunguzia mzigo wafanyakazi ambao ni rahisi kuwafuatilia, lakini Kariwa alisema idadi ya wafanyakazi katika sekta rasmi ni ndogo na hivyo hawawezi kulipa kodi za kutosheleza mahitaji ya kuendesha nchi.

Kuhusu Wizara ya Kazi kutotangaza maamuzi yake kuhusu mapendekezo ya utafiti unaohusu kima cha chini katika sekta binafsi, Kariwa alisema hakuna sheria inayounda taasisi ya kutafiti kima cha chini vya mishahara.

“Taasisi zilizopo ni bodi za kisekta za mishahara ambazo zina jukumu la kushauri juu ya kima cha chini cha mishahara. Dai la Tucta hapa ni kuhusu kutangazwa kwa mapendekezo ya mshauri mwelekezi ambaye ni Taasisi ya Utafiti wa Uchumi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Economic Research Bureau).

“Tunachojua ni kwamba taarifa ya utafiti wa Mshauri Mwelekezi pamoja na maoni ya bodi za kisekta za mishahara yalijadiliwa katika kikao cha mwisho cha Baraza la Ushauri la Uchumi na Jamii (LESCO) lililokutana Machi 25, 2010. Tucta iliwakilishwa katika kikao hiki,” alisema Kariwa.

Kuhusu Wizara ya Kazi kushindwa kuunda bodi mpya za mishahara za sekta binafsi tangu zile za zamani zilipomaliza muda wake Aprili mosi, 2009, alisema bodi za mishahara za kisekta kama vilivyo vyombo vingine vya utatu vinavyoteuliwa chini ya sheria ya Taasisi za Kazi, (Na. 7 ya 2004) vilipewa uhai wa miaka mitatu toka kuundwa kwao.

“Bodi za mishahara za kisekta ziliundwa Aprili 2007 na hivyo ukomo wake utaishia mwezi huu na si kweli kwamba uhai ulikoma Aprili 2009 kama Tucta inavyodai. Tucta inatambua kwamba mchakato wa kuundwa upya kwa bodi hizi umeanza tangu Machi, 2010 na hivyo hii haiwezekani kuwa hoja ya kusababisha mgomo,” alisema Kariwa.

Kuhusu Wizara ya Kazi kushindwa kuitisha vikao vya Lesco ambacho ni chombo cha kuishauri serikali kuhusu masuala ya wafanyakazi tangu chombo hicho kizinduliwe mwezi Agosti 2009, Kariwa alisema pamoja na sheria kutofafanua lakini chombo hicho kinapaswa kukutana mara tatu kwa mwaka.

“Lwsco ilizinduliwa Agosti 2009, inabidi ifikapo Agosti mwaka huu iwe imekutana angalau mara tatu. Mpaka sasa imeshakutana mara mbili na bado tuna miezi minne kufikia Agosti,alisema.

Akizungumzia kuhusu serikali kutokuwa makini katika kurekebisha malipo dhaifu yatokanayo na Mifuko ya Pensheni ya wastaafu hivyo kuwafanya wastaafu wengi kupata mafao duni ya uzeeni, alisema mchakato wa kurekebisha matatizo yaliyopo katika mifuko hiyo ulishaanza.

Hata hivyo, ATE imeiomba Tucta kushiriki kwa dhati katika majadiliano yenye lengo la kutafuta muafaka.

“Kwa hili hakuna njia ya mkato. Tucta itambue kwamba majadiliano baina ya wadau yanajenga hali ya kuaminiana na mahusiano mazuri na endelevu,” alisema.

Taasisi zilizokopesha walimu kinyemela zabanwa

TaboraTAASISI za fedha mkoani hapa ambazo ziliingia mikataba ya mikopo na wafanyakazi bila kumshirikisha mwajiri zimetakiwa kusitisha mara moja makato vinginevyo zitachukuliwa hatua za kisheria.

Baraza la Wafanyakazi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui lililokutana juzi mjini hapa, limeziagiza taasisi hizo kusimamisha mara moja makato hayo baada ya kitendo chao cha kukaidi kuitika wito wa mwajiri wa watumishi 166 wa halmashauri hiyo aliyeagiza kukutana na wahusika wake wanaoonekana kutojali.

Kwa kauli moja wajumbe wa kikao hicho walisema lengo la kusitisha makato hayo ni kuzilazimisha taasisi hizo za fedha kuwasilisha mikataba yao kwa mwajiri, ili kuhakiki kama ilifungwa kwa kuzingatia taratibu za kisheria.

Taasisi ambazo zinahusika na hoja hiyo ni Faidika, Bayport, Blue Financial Service, Tunakopesha na Istant Credit ambazo ziliandikiwa barua Agosti 11 mwaka jana lakini hazijajibu hali ambayo inadhihirisha wazi kwamba mikataba hiyo haikufuata taratibu za kisheria.

Imefahamika watumishi hao 166 ambao ni walimu waliingia mikataba ya mikopo na taasisi hizo pasipo hata kumshirikisha mwajiri, hali ambayo inawaletea shida ya kipato kwani utakuta wengi wao wamekuwa wakiambulia chini ya robo ya mshahara.

Katika hatua nyingine, viongozi wa Chama cha Akiba na Mikopo cha Walimu Wilaya ya Uyui, wameaswa kutekeleza majukumu yao kwa uwazi ikiwemo kufuata kanuni, taratibu na sheria za vyama vya ushirika zinazowaongoza.

na Murugwa Thomas,

Saturday, April 3, 2010

DEDICATION

To my almighty God for making me who i am.My Grandfather mzee BILINGI FULGENCE my big brothers and sisters ROBERT SHIMA,BUGUHE EMMANUEL,MASEMBA.R,THOMAS MUSWAGA(the great),CHARLES SAGUDA,MARUGU FAUSTINE,MADHARA.M,DOMINICK S.MAJENGO(the king)GRACE MMBANDO(iron lady),VERONICA ZABLON,MAGRETH MHANGWA, and JOHARI KAPAYA.Thank you for your patience,prayers,moral and material support which to me are not measurable.You have been the light and footprints to me.Much love to you.

from CHINYULI D.E

TUCTA YAMVIMBIA JK

YASEMA KUAHIDI ONGEZEKO LA MSHAHARA NI KUVUNJA SHERI

SHIRIKISHO la Vyama Vya Wafanyakazi (Tucta) limekataa wito wa Rais Jakaya Kikwete wa kutaka wamalize matatizo yao kwa njia ya mazungumzo, likisema labda mkuu huyo wa nchi aitishe kikao kitakachowahusisha watendaji wake.

Tucta imeshatangaza kuwa mgomo huo wa nchi nzima utafanyika kuanzia Mei 5 na kwamba haitamwalika rais siku ya sherehe za Mei Mosi na badala yake mwenyekiti wa shirikisho hilo ndio atakuwa mgeni rasmi na siku hiyo itatumika kuzungumzia matatizo ya wafanyakazi na mgomo.

Tucta inadai kuwa kwa muda mrefu serikali imepuuza madai ya wafanyakazi ambayo ni pamoja na ongezeko la mshahara, kupunguziwa kodi inayokatwa kwenye mishahara, malipo kidogo kwa wastaafu na wizara kushindwa kuitisha mikutano ya Lesco.

Lakini Rais Kikwete alijibu madai yao kwa kuwasihi viongozi wa Tucta kukubali kukaa mezani ili matatizo hayo yaishe kwa mazungumzo na kwamba serikali iko mbioni kupandisha mishahara licha ya ufinyu wa bajeti.

Jana naibu katibu mkuu wa Tucta, Nicolaus Mgaya alisema kuwa Rais Kikwete amedanganywa na mawaziri wake kuhusu chanzo cha mgomo huo na hivyo hotuba yake juzi haikujitosheleza.

"Tumepokea hotuba yake na maombi yake tumeyasikia, lakini tunasikitika kuwa mambo mengi aliyoyazungumza yanaonyesha mawaziri wake wanamdanganya, njia pekee ni kwa yeye kukutana na sisi katika mazungumzo ambayo yatahusisha mawaziri wake ili tuyawake bayana mambo hayo," alisema

Alifafanua kuwa katika hotuba hiyo, rais anaonekana alidanganywa kuwa Tucta ilikutana na Tume ya Utumishi wa Umma katika vikao vya majadiliano mara sita, wakati si kweli. Alisisitiza kuwa hawakutana katika kikao chochote na tume hiyo.

Mgaya alimshambulia Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi wa Umma), Hawa Ghasia na Waziri wa Kazi Ajira na Maendeleo ya Vijana, Juma Kapuya kuwa ndio wanaompotosha rais kwa kutomweleza ukweli kuhusu suala hilo.

Mgaya alifafanua kuwa katika hotuba yake ya juzi rais alizungumzia dai moja kati ya madai matatu na akaipinga ahadi ya mkuu huyo wa nchi ya kupandisha mshahara, akidai kuwa kuahidi kwa jinsi hiyo ni kinyume na sheria.

"Sheria inataka kuwapo kwa majadiliano baina ya wafanyakazi na waajiri wake juu ya suala la kupandishwa kwa mishara na madai mengine kabla ya kutekelezwa kwake majadiliano hayo ambayo huhitimishwa Desemba 15 yanalenga kutoa fursa kwa vipengele vya makubaliano kuingizwa kwenye bajeti.

"Vikao hivyo havijafanyika leo tunakwenda kujadili nini wakati bajeti ya kwa mwaka huu iko tayari," alisema Mgaya.

Kwa mujibu wa Mgaya, kitendo cha Rais Kikwete kuwaeleza kuwa atapandisha mshahara bila kuwapo makubaliano ni kinyume na sheria kwa kuwa maamuzi hayo yanahusu upande mmoja na yanaweza kutoa mwanya kwa serikali kulipa mishahara midogo kinyume na matarajio ya wafanya kazi.

Alisema kimsingi ili mshahara upandishwe, majadiliano baina ya wafanyakazi na waajiri yanatakiwa na kwamba baadhi ya vipengele vitakavyotokana na majadiliano hayo ndivyo vitakavyoingizwa kwenye bajeti kwa ajili ya kuombewa fedha.

Mgaya alisema kitendo cha rais kutoyazungumzia madai mengine ya wafanyakazi kwenye hotuba yake ni ishara nyingine kwamba hajaelezwa kila kitu kinachosababisha maandalizi ya mgomo huo yanayosimamiwa na mwenyekiti wa kamati, Gratian Mukoba.

Alitaja madai mengine kuwa ni malipo kidogo wanayoyapata wafanyakazi wanapostaafu kutoka kwenye mifuko ya kijamii na kodi kubwa wanayotozwa wafanyakazi kutoka kwenye mishahara yao.

Alisema walishatoa ushauri mara kadhaa kwa serikali kupanua wigo wa kukusanya kodi ili kupunguza mzigo kwa wafanyakazi kwa kuwa kuna kundi la Watanzania ambao hawalipi kodi, lakini serikali haijashughulikia.

Mwenyekiti wa kamati ya mgomo huo, Gratian Mkoba alisema kwa sasa wafanyakazi hao hawako tayari kurudi kwenye meza ya mazungumzo na serikali kwa kuwa mgomo huo umefuata taratibu zote.

Kuhusu hutuba ya rais iliyotolewa juzi alisema wafanyakazi hawajaridhika nayo na kusisitiza kuwa hawawezi kurudi nyuma, labda madai yao yaingizwe kwenye bajeti ya mwaka huu.

"Ingawa tunaingia kwenye kikao kujadili suala hilo kwa sasa bado inaonekana hotuba ya rais haijaturidhisha... wafanyakazi hatujaridhika nayo; kwanza imetuongezea ajenda kwenye kikao chetu. Sisi hatutakuwa tayari kubadili msimamo wetu labda tuhakikishiwe kuwa madai hayo yanaingia kwenye bajeti ya mwaka huu," alisema Mukoba.

Juzi Rais Kikwete alikiri kuwa imekuwa inamuwia vigumu kuzungumzia mgomo wa wafanyakazi wote ulioitishwa na Tucta na akaenda mbali zaidi kuwasihi viongozi wa wafanyakazi kufikiria upya uamuzi wao.

Pia mkuu huyo wa nchi ameeleza kwa msisitizo kuwa serikali haipuuzi madai ya wafanyakazi, bali "tunawajali na kuwathamini sana wafanyakazi: wawe wa serikali au wawe wa sekta binafsi" na hivyo kuwasihi viongozi wa Tucta kukubali kufanya mazungumzo na serikali na waajiri wengine ili kumaliza mgogoro huo.

Rais Kikwete alionyesha unyenyekevu akiwasihi wafanyakazi kufanya mazungumzo kwa kuwa ndio uamuzi wenye maslahi kwa taifa badala ya kutumia mgomo.

"Lazima nikiri mapema kabisa kuwa nilipata taabu kulizungumzia jambo hili hasa kwa jinsi kauli za viongozi wa vyama vya wafanyakazi wanaohamasisha mgomo huo zilivyokuwa kali," alisema Kikwete katika hotuba yake.

Friday, April 2, 2010

SPECIAL GREETINGS


HOW ARE YOU DOING GUYS?, NAFIKIRI MTAKUWA POA.SINA MENGI LICHA YA KUWAKOSA KUPITA KIASI NILITAKA KUWATAKIA PASAKA NJEMA .

Vodacom yatoa msaada wa kompyuta 20 meatu secondary

Kampuni ya Simu za mkononi ya Vodacom- imetoa msaada wa kompyuta 20 kwa shule mbili za sekondari za Samuye na Meatu mkoani Shinyanga .

�Mkuu wa kanda ya ziwa wa kampuni hiyo Bwana Stephen Kingu ameseme msaada huo umetolewa na kampuni yake kupitia kitengo chake cha misaada kwa jamii.

Amesema lengo ni kuwawezesha wanafunzi wa shule hizo kujifunza masomo ya kompyuta ili wawe na uwelewa mpana wa teknolojia ya habari na mawasiliano.

Naye Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Kanali Mstaafu Edmund Mjengwa amewataka wanafunzi wa kike wa shule za sekondari mkoani humo kujiepusha na upokeaji wa zawadi ndogo ndogo zenye ushawishi kutoka kwa wanaume kwa lengo la kuwataka kimapenzi.
  • SOURCE: Radio One

Thursday, April 1, 2010

mbunge wa Kishapu Fred Mpendazoe kukihama Chama Cha Mapinduzi








Waandishi Wetu

HATUA ya mbunge wa Kishapu Fred Mpendazoe kukihama Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kujiunga na Chama Cha Jamii (CCJ) imekipa kiwewe chama hicho tawala baada ya makada wake kutoa kauli zinazoashiria kumkebehi huku Ridhiwan Kikwete akiwatoa hofu wanachama wa chama chake.

Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Katibu wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Mohammed Mbonde, aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Wenyeviti wa mikoa wa CCM, Pancras Ndejembi, mtoto wa Rais Kikwete, Ridhiwan na wapigakura wa Jimbo la Kishapu jana walitoa kauli zinazotofautiana kuhusu uamuzi huo wa kihistoria.

Mjumbe wa Baraza Kuu la UVCCM, Ridhiwan Kikwete alisema kujiondoa kwa Mpendazoe kumeonyesha kuwa wananchi walikuwa na mbunge wa aina yake na kuwasihi wamwache aende zake.

Ridhiwan ambaye alikuwa katika ziara ya siku mbili mkoani Shinyanga kuhudhuria sherehe za kusimikwa kwa makamanda wa UVCCM wa wilaya, ziara ambayo imefanyika siku moja baada ya mbunge huyo kutangaza kuihama CCM na kujiunga na CCJ.

Alisema kuondoka kwa mbunge huyo kutoka CCM na kukimbilia CCJ ni kielelezo cha aina ya viongozi ambao wamekuwa mzigo kwa chama ambao wamekuwa wakipendekezwa na kuteuliwa kuongoza.

"Mwacheni aende Mpendazoe, kuondoka kwake kusitufanye kukosa raha sisi CCM, wapo wengi waliondoka na chama bado kipo imara, muhimu kusonga mbele,� alieleza.

Alisema Mpendazoe alikuwa akifanya mambo mengi kinyume na kanuni za chama na kuwaomba wananchi kutulia na kuangalia viongozi wengine, lakini akisisitiza kuwa walio makini na siyo wale wa kuja.

Ridhiwan alisema kuondoka kwa Mpendazoe kunapaswa kuwa fundisho kwao kuchagua viongozi wenye sifa za uongozi na wenye uwezo wa kuongoza na kutamba kuwa chama kinao wanachama wengi, hivyo wanaoondoka kwa sababu zao wajue kuwa CCM itaendelea kubaki pale pale bila ya kutetereka.

“Nawaasa viongozi kutochagua viongozi kwa kuangalia sura au fedha za mtu, bali chagueni watu wenye moyo na msimamo wa kukitetea na kuimarisha chama kwa vitendo…, huo ndio msimamo wa CCM,� alisisitiza Ridhiwan.

Awali kabla ya kuongea kwa Ridhiwan, UVCCM Shinyanga, ulitoa tamko ambalo lilisomwa na Gasper Kileo la kusema kuwa vijana wa chama hawawezi kunyamaza kimya kutokana na kitendo cha mbunge huyo kujiengua CCM.

Walisema kuwa kwa muda mrefu mwenendo mzima wa mbunge huyo ulikuwa na mwelekeo wa kukinzana na maadili ya CCM, na kwamba alichokifanya ni kukipunguza mzigo kwa vile tayari alikuwa kero ndani ya chama na jimbo lake kwa ujumla.

“Hatukujua kama tuliteua mbunge asiyekuwa na uchungu na wapigakura wake kiasi cha kuwatelekeza na kuwanyima haki yao ya kuwa na mwakilishi hasa katika kipindi hiki cha bajeti, tunaamini hakuna kitakachoharibika kwani tunatambua mshikamano wa watu wa Kishapu’’ alisema kada huyo katika tamko hilo la vijana.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Hamisi Mgeja, yeye alimkana Mpendazoe kwamba hakuwa kiongozi ambaye alipatikana katika mchakato wa uchaguzi yeye akiwa ni mwenyekiti bali walimkuta baada ya kupitishwa na viongozi wenzake waliowatangulia.

Alisema viongozi wenzake walikosea kumteua Mpendazoe kwa vile alifahamika na kwa kufanya kwao hivyo waliwaacha wengine wenye uwezo ambao kama wangepewa nafasi ya Mpendazoe leo bado wangelikuwa wakiendelea kuwatumikia wananchi wa Kishapu.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani Kishapu, Boniface Butondo alipohojiwa na Mwananchi alisema kuwa kuondoka kwa Mpendazoe kumewafanya kupumua kwa vile alikuwa kero kubwa na mwenye ugomvi jambo ambalo lilimfanya kutofautiana na madiwani walio wengi wa chama chake.

Hata hivyo, katika hafla hiyo fupi ya kuwasimika makamanda wapya wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga, zilizofanyika kwenye Viwanja vya NSSF mjini, jumla ya makamanda 17 walisimikwa na Ridhiwan Kikwete kwa ajili ya wilaya za Kahama, Bariadi, Bukombe Maswa, Meatu, Shinyanga mjjini, Shinyanga Vijijini na Kishapu iliyokuwa Jimbo la Mpendazoe.

Naye Mbonde jana aliripotiwa na vyombo vya habari kuwa alimwandikia barua Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba kumweleza kuwa CCM Shinyanga ilitarajia hatua hiyo ya Mpendazoe siku nyingi hivyo kilichotokea ni sawa na kuvuja kwa pakacha ambako ni nafuu ya mchukuzi.

Kwa mujibu wa barua hiyo yenye kumbukumbu namba CCM/SHR/CON.2/Vol.IV/157, katibu huyo wa mkoa alisema CCM Shinyanga ilitarajia hilo kutokana na minong'ono ya muda mrefu na mabadiliko ya tabia na mwenendo wake uliojidhihirisha katika matamshi yake ndani ya Bunge na jimboni Kishapu.

"Mheshimiwa katibu nikuhakikishie kwa dhati kabisa kuwa Jimbo la Kishapu ni mali ya CCM na ngome kuu ya chama chetu. Usishtuke sana kwani kuvuja kwa pakacha ni nafuu kwa mchukuzi. Aende salama," ilinukuliwa taarifa hiyo.

Wakati katibu huyo akitoa kauli hiyo, mwanasiasa nguli nchini, Mzee Ndejembi alisema uamuzi wa Mpendazoe kuihama CCM haujakipunguzia kitu chama hicho.

Kauli hiyo ya Ndejembi inafanana na kauli iliyotolewa juzi na Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa.

Lakini jana Ndejembi aliongeza kuwa uamuzi wa mbunge huyo unaonyesha kuwa CCM inakubalika kila kona ya nchi akiwataka wengine ambao wako kimasilahi waondoke mapema kama alivyofanya Mpendazoe.

“Mimi nasema CCM kitaendelea kuwa ngangari na watapondwa vipande vipande katika Uchaguzi Mkuu wala watu wasitishwe na huyo Mpendazoe kwani kufanya hivyo amekiimarisha chama na kukiweka katika mazingira mazuri sana kuelekea uchaguzi � alisema Ndejembi na kuongeza:

“CCM inaongozwa kwa mujibu wa Katiba, kanuni na taratibu na hata wao walikikuta na wamekiacha na hao waliingia kwa kufuata masilahi sasa wameona malengo yao hayatimizwi kutokana na misimamo iliyopo ndani yake.�

Ndejembi alisema wapo viongozi ambao walihama CCM, lakini hadi leo chama hicho kimesimama na hakiyumbi na kuwatolea mfano kina Lipumba na Seif Sharif Hamad (CUF) ambao kuondoka kwao hakukuyumbisha chama.

Hata hivyo, alionyesha wasiwasi kuwa labda kuna jambo lililomsibu mbunge huyo mpaka akaihama CCM kwani uamuzi huo ni mzito mno kufanywa na mtu wa hadhi yake.

“Mtu mzima kulia barabarani lazima kutakuwa na jambo ama msiba au ameibiwa,� hivyo na Mpendazoe inawezekana moja kati ya hayo limemkuta.

Kiongozi mkongwe katika medani ya siasa nchini, Peter Kisumo ameeleza kuwa pamoja na jitihada za Rais Jakaya Kikwete kuweka sheria mbalimbali za kudhibiti vitendo vya rushwa bado kuna baadhi ya wabunge ndani ya chama hicho wanatoa rushwa ili wapate uongozi.

Alisema Serikali ya Awamu ya Nne imejitahidi kupingana na kadhia za rushwa hasa katika nyanja ya siasa, lakini, kutokana na sababu mbalimbali sheria hiyo itakuwa ngumu kutekelezwa hasa kwa baadhi ya viongozi waliyopo ndani ya CCM.

Mzee Kisumo alitolea mfano wa hivi karibuni wa baadhi ya wabunge kukiri kutoa vyakula na posho za nauli kwa baadhi ya wanachama wa CCM na hata kuwanunulia mavazi akieleza kuwa mambo hayo ndiyo yatakayofanya sheria hiyo ikose nguvu.

Alidai kuwa katika Mkoa wa Kilimanjaro kuna kiongozi mmoja mkubwa ambaye kila wiki anafanya sherehe na kutoa zawadi mbalimbali kwa wanaofika kumuunga mkono jambo ambalo linahitaji kutolewa kwa elimu juu ya sheria hiyo mpya kabla ya kuanza kutumika.

Alisema kuwa kitendo cha Rais Jakaya Kikwete kufanikisha kuwepo kwa sheria hiyo kunamfanya aonekane kuwa ni miongoni mwa viongozi wenye kujiamini na kutoa mfano kwa viongozi wengine ndani na nje ya Tanzania .

Kwa upande wao baadhi ya wananchi wa wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga wamepongeza uamuzi wa mbunge wao kuihama CCM na kujiunga na CCJ.

Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti jana walisema CCM sasa kimepoteza dira na kuwakumbatia mafisadi.

Walisema uamuzi huo ni wa busara kwani kwa muda mrefu Mpendazoe alipingwa na viongozi wa CCM wa ngazi zote kutokana na msimamo wake wa kupinga ufisadi.

Walisema licha ya mbunge huyo kujitahidi kuwaletea maendeleo katika jimbo hilo, lakini juhudi zake zimekuwa zikikwamishwa na viongozi wa CCM kwa kushirikiana na viongozi wa serikali hasa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga kwa kumfanyia majungu ili aonekane hafai kwa wanannchi.

“Mpendazoe amejitahidi sana kuhamasisha shughuli za maendeleo katika jimbo hili ambalo ni wilaya mpya, lakini juhudi zake zote zimekuwa zikikwamishwa na viongozi wa CCM kwa kushirikiana na baadhi ya viongozi wa serikali hasa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga na hivyo kumfanyia majungu ili tumuone hafai,� alisema Asha Juma.

Walisema mbunge huyo amekuwa akiandamwa na mambo mbalimbali ambayo hayana msingi hata kuzuliwa kesi ili aweze kupatikana na hatia na hatimaye kufungwa na kupoteza sifa ya kugombea ubunge katika jimbo hilo.

Pia waliongeza kwa kueleza kuwa uongozi wa CCM Mkoa wa Shinyanga ulikuwa ukisambaza vipeperushi vya kumkashifu mbunge huyo katika maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo ambapo hufanyika minada kila juma lengo kubwa ni kumchonganisha na wapigakura.

Aidha, walisema CCM ilikuwa imemwandaa mfanyabiashara mmoja maarufu mwenye asili ya Kiasia kuchukua nafasi yake.

Walisema viongozi wa CCM Mkoa wa Shinyanga hawataki wabunge wasomi na wenye msimamo unaosimamia ukweli kutokana na kuzoea vitendo vya ubadhirifu kwa kuwa wengi wao walikuwa viongozi ndani ya Chama cha Ushirika Mkoa wa Shinyanga(SHIRECU)ambacho kimefilisika kutokana na matumizi mabaya.

Habari hii imeandaliwa na Habel Chidawali, Dodoma, Suzy Butondo, Samwel Mwanga-Shinyanga, Hemed Kivuyo, Arusha.

MPENDAZOE Januari: CCM ‘Damdam’ Machi: ‘Damdam’ CCJ

BAADA ya Januari mwaka huu kuhojiwa na wanahabari kuhusu uvumi wa kujiunga na Chama Cha Jamii (CCJ) akakana, aliyekuwa Mbunge wa Kishapu kwa tiketi ya CCM, Fred Mpendazoe, ametangaza rasmi kujiunga na chama hicho.

Akihojiwa na gazeti hili mwanzoni mwa mwaka huu, kuhusu CCJ na uhusiano wake na viongozi wa chama hicho, Mpendazoe ambaye amekuwa pamoja na baadhi ya wabunge wakijinadi kupambana na ufisadi nchini, alisema: “Siwezi kuzungumzia mambo ya CCJ kwa sababu mimi ni CCM na huyo Mubhi (Renatus - Katibu Mkuu wa muda) si ndugu yangu na nasikia anatoka mkoa wa Mara … hata angekuwa ndugu yangu kuna tatizo? Mbona Slaa (Wilbrod) yuko Chadema na mkewe CCM na wanaishi pamoja? Kila mtu ni mtu mzima.” Aliongeza kusema yeye bado ni mwana CCM na ni mwakilishi wa watu na wanaomhusisha na CCJ wanaweza kuwa na nia yao mbaya.

Lakini akitangaza Dar es Salaam jana kuhama CCM, mbunge huyo wa zamani alisema: “Nimefuatilia kwa karibu na kusoma Katiba ya CCJ. Nimeishi kwa matumaini kwa muda mrefu, nikitarajia siku mambo yatabadilika ndani ya CCM, mpaka leo sioni dalili yoyote. Nimeona ni heri niheshimu dhamira yangu, kama Mwalimu Julius Nyerere, alivyotuasa kuwa CCM si Helena (mama yake mzazi).

”Nasononeka CCM imegeuka kimbilio la kila mwenye dhamira ya ulanguzi, CCM imepoteza maadili ya uongozi na imekuwa ngome ya mafisadi wanaotafuna utajiri wa nchi yetu.”
Aliongeza: “CCJ ni kama Yoshua aliyewapeleka Kanani. Hakuna ubishi CCM imetutoa Watanzania katika Ukoloni, imefanya kazi kubwa, imefikia kilele chake lakini nasema haiwezi tena kuwapeleka Watanzania kwenye mabadiliko ya karne hii, tunahitaji fikra na mtazamo mpya ambao haina.

CCJ ndiyo itakayotupeleka kwenye mabadiliko ya kweli na ya dhati.” Wabunge wengine wa CCM ambao walikana kuhusishwa na CCJ ni pamoja na John Shibuda (Maswa), Anthony Diallo (Ilemela) na Dk. Harrison Mwakyembe (Kyela). Vigogo wengine waliokana ni Mawaziri Wakuu wa zamani, John Malecela na Joseph Warioba. Naye Mubhi kwa upande wake, alikana kuwa na uhusiano na Mpendazoe, akisisitiza kuwa hata hamfahamu.

Mwenyekiti wa CCJ, Richard Kihabo alisema jana kuwa Mpendazoe amejiunga na chama chake si kwa sababu ya kutafuta cheo, bali kutoa mchango wake katika mustakabali wa maendeleo ya Taifa. “Ametangaza kujiunga na chama kwa lengo la kutoa mchango wake na si kufuata cheo hapa, mtu yeyote anayetaka kujiunga na chama anaruhusiwa ili mradi asivunje sheria,” alisema. Kwa upande wa CCM, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa, alisema chama chake kimezisikia taarifa hizo kijuujuu, lakini kwa mujibu wa Katiba Ibara 13 (1) (a) mwanachama yeyote akijiunga na chama kingine amejivua uanachama CCM.

Alisema CCM pia inatambua kuwa ni haki ya mwanachama awe kiongozi au la, kuhama chama na kwenda kingine. “Na huyu Mpendazoe ametumia haki yake hiyo, CCM tuna wanachama zaidi ya milioni 4.6 hivyo hatotuathiri kuondoka kwake,” alisema.

Katibu wa Bunge, Thomas Kashilillah alisema kwa mujibu wa Katiba ya nchi Ibara ya 71, mbunge anapohama chama anapoteza moja kwa moja sifa ya kuwa mbunge. “Kwa lugha ya kibunge huwa tunaita crossing floor, hapo hupoteza ubunge na sifa zake zote,” alisema.

Alisema taarifa za Mpendazoe kujiunga CCJ wamezipata lakini si rasmi na chama chake cha awali cha CCM ndicho chenye jukumu la kutoa taarifa katika Ofisi za Bunge, kuhusu kujiondoa kwa mbunge huyo. Hata hivyo, Msekwa alipingana na hilo na kutoa mfano wa Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour (TLP) Augustine Mrema, ambaye akiwa mbunge wa Moshi Vijijini alihama CCM na kujiunga na NCCR-Mageuzi.

“Haikuhitajika kupelekwa taarifa, tamko alilotoa kwenye mkutano wa hadhara lilitosha kabisa kumwondolea sifa ya ubunge, hali ambayo ni sawa na hii ya Mpendazoe ambaye leo (jana) tumemsikia ametangaza mwenyewe tena hadharani kujiondoa CCM, inatosha kabisa kumwondolea sifa ya ubunge.” Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi (NEC), Rajab Kiravu, alisema hata kama mbunge huyo atakuwa amejiondoa na chama kilichompitisha kuridhia na jimbo kuwa wazi, nafasi hiyo haitazibwa mpaka uchaguzi mkuu wa Oktoba.

Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila, hakuwa tayari kusema lolote badala yake alimpa jukumu hilo Ofisa Habari Mwandamizi wa Bunge, Ernest Zulu, ambaye kama bosi wake, hakuwa tayari kuzungumza zaidi.

“Ninachoweza kusema hapa ni kwamba ofisi ya Bunge inasubiri barua kutoka wale waliowaletea orodha ya Wabunge ambao ni Tume ya Uchaguzi.” Naibu Spika wa Bunge, Anne Makinda aliyetakiwa kuzungumzia haki za mbunge anayehama chama, ikiwamo hatma ya mafao yake, alisema hawezi kuzungumza lolote kwa kuwa alikuwa safarini.

“Nipo huku porini na sikusikii vizuri na nimechelewa utanisamehe.” Mbunge wa Kahama, James Lembeli (CCM), alisema amepokea uamuzi wa Mpendazoe kwa mshtuko mkubwa na ataamini jambo hilo atakapoambiwa na Mpendazoe mwenyewe.

“Mpendazoe amekuwa karibu sana nami na hakuwahi kunielezea azma yake ya kuondoka CCM,” alisema Lembeli. “Kwa hali ya kawaida kuhama chama sasa hivi ni jambo zito, uamuzi wake ni sawa na mtu anayeamua kujinyonga anafikia hatua ya kufanya hivyo baada ya kuona hakuna suluhisho lingine,” alisema.

Naye Mbunge wa Nzega, Lucas Selelii (CCM), alisema amesikitishwa na uamuzi huo kwani ni habari mpya na ngumu kwake na hata kuelezea inakuwa ngumu. Selelii alipoulizwa kama na yeye ana nia hiyo alisema, “wapo watakaokwenda huko lakini si mimi … mimi ni mwanachama wa CCM na nitaendelea kubaki CCM hata kama si kiongozi.”

Lucy Owenya (Chadema) alisema, “kama kaamua kuhama Katiba inamruhusu…huyu anajua matatizo yaliyoko ndani ya CCM ndiyo maana kaamua kuondoka,” alisema Owenya.

Elieta Switi (CCM), alisema kuhama ndiyo maana halisi ya demokrasia, kwamba mtu habanwi kuwa katika chama kimoja na kuongeza, “kazi ni kwake huko alikokwenda, lakini nadhani yeye anaona amefanya uamuzi sahihi na ana sababu ya kufanya hivyo”.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, kupitia mtandao wa kompyuta alisema ni uamuzi wa kishujaa kwamba anaweza kutoka na kujiunga na kambi ya Upinzani.

“Tunamkaribisha. Nina shaka na 'strategy (mkakati)' ya kutoka kwa kuzungumza na waandishi wa habari pale MAELEZO na si mkutano jimboni mwake maana hatakuwa mbunge tena kwa kipindi kilichobaki. “Inawezekana amenusa kitu kuwa jamaa wanamtosa, maana nimesikia kulikuwa na Kamati Kuu ya CCM,” alisema.

Kuhusu mafao, alisema hukokotolewa kwa mujibu wa muda ambao mbunge ametumikia. Hata mbunge akifariki dunia sehemu ya mafao yake hulipwa kwa familia yake.

Mbunge mwingine ambaye hakutaka kutajwa jina, alisema huenda Mpendazoe amehisi kuwa hatapita katika kura za maoni CCM, kutokana na madai kuwa matajiri wameshammaliza, hivyo atapitia CCJ kuwania ubunge.

Kabla ya kuhama CCM, Mpendazoe amekuwa akikabiliwa na vitimbi mbalimbali jimboni mwake, ikiwa ni pamoja na kusambazwa vipeperushi kwenye mnada wa mifugo na mitaa ya mji mdogo wa Mhunze, wilayani Kishapu, vikimtuhumu kwa kutotimiza ahadi zake.

Baadhi ya vipeperushi vilisomeka: 'Mpendazoe ulitudanganya kuwa tukikuchagua ubunge utateuliwa kuwa Waziri, mbona hata unaibu Waziri hukuteuliwa!' 'Mpendazoe wananchi wa Kishapu hatukutaki uwe mbunge wetu, ukigombea tena 2010 tutakuaibisha!

Vingine: ‘Mpendazoe umeivuruga halmashauri ya wilaya ya Kishapu sasa unataka kukivuruga Chama Cha Mapinduzi, chunga kauli zako’. Hata hivyo akivizungumzia, alisema ni sehemu ya utekelezaji wa mafisadi kuwaondoa bungeni baadhi ya wabunge wanaopinga vitendo hivyo.

Alidai mafisadi wametenga Sh bilioni mbili kwa ajili ya kuwang’oa na kuwamaliza wasisikike kabisa. Hata hivyo, alisema hatishiki na vipeperushi hivyo, kwa kuwa wanaovisambaza wamefilisika kisiasa na ni woga kwa kuwa hawajitokezi hadharani na kwenye vikao halali kutoa madukuduku yao.

Alijinasibu kuwafanyia mambo mengi wapiga kura wake na akawa na imani kuwa wananchi hao watavipuuza na kuendelea kumuunga mkono. Habari zaidi zilidai kuwa mbunge huyo alisababisha kuibuka makundi mawili jimboni mwake; linalomuunga mkono na linalompinga, huku ikidaiwa kuwa alishitakiwa kwa Spika Samuel Sitta na aliyekuwa msaidizi wake katika uchaguzi wa mwaka 2005 kwa madai ya kumdhulumu.

Katika kukanusha tuhuma hizo, Mpendazoe alikiri kufahamiana na msaidizi wake huyo na kusema alishamsaidia mambo mengi, lakini hakumlipa fedha zake kutokana na kumchafua na kutoa siri zake sehemu mbalimbali.

“Huyo bwana namjua ni ndugu yangu, ni kweli tulikuwa na makubaliano fulani ambayo mimi sijayatekeleza, lakini ameniudhi sana baada ya kuzunguka sehemu mbalimbali na kuanza kutoa siri zangu,” alikaririwa na gazeti moja nchini.

“Kote alikokwenda wamempuuza, amefika hadi kwa Spika, NEC, PCCB hadi Polisi ili kunichafua, lakini wamempuuza, sasa anatumia vitisho ili nimlipe, kwa nini?” Mpendazoe pia alituhumiwa kumtisha kwa bastola Abdulkadir Mohamedi, ambaye pia ni kada wa CCM Kishapu.

Ilidaiwa kuwa Mbunge huyo wa zamani alimshambulia Mohamedi kwa makofi, kumchania nguo na kumtishia bastola, lakini alikanusha akidai ni uongo dhidi yake wenye lengo la kumchafua kisiasa.

Tigo sasa nusu shilingi kwa sekunde

na Mwandishi Wetu


KAMPUNI ya simu za mkononi ya Tigo imezindua huduma ya nusu shilingi ambayo itapatikana kwa wateja wate wa Tigo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Ofisa Uhusiano wa Tigo, Jackson Mmbando, alisema kuwa wateja wote wa Tigo wataweza kufurahia huduma hiyo baada ya dakika ya kwanza ya muda wa maongezi.

“Tigo kama kawaida yetu, leo tunawaletea huduma nyingine nzuri zaidi na lengo ni kumwezesha Mtanzania kupata mawasiliano kwa gharama nafuu kabisa. Sasa mteja wa Tigo ataweza kuzungumza kwa nusu shilingi (thumni) baada ya dakika ya kwanza ya muda wa maongezi,” alisema.

Alisema kwa kufanya hivyo Tigo imerudisha thamani ya thumni katika matumizi ya pesa na kuongeza kuwa huduma hiyo ni ya kudumu.

“Kampuni ya Tigo ndiyo inayoongoza kwa kutoa gharama nafuu kwa watumiaji wake na huduma hii inakuwa ni kwa saa 20 kuanzia saa 12 asubuhi hadi 12 jioni na kuendelea tena saa 4 usiku hadi saa 12 asubuhi,” alisema.

Aliongeza kuwa huduma hiyo ni kwa wateja wa Tanzania Bara na kusema kuwa wateja wao wa visiwani wanaendelea kufaidi huduma ya robo shilingi kwa dakika, ambayo imezinduliwa hivi karibuni visiwani hum




ICS yatumia milioni 226 Meatu
Shirika lisilo la kiserikali la International Child Support (ICS) limetumia kiasi cha sh 226, 386, 500 wilayani Meatu mkoani Shinyanga, kwa kipindi cha mwaka 2004/ 2005 kutekeleza mpango wa kusaidia mtoto shuleni.

Hayo yalisemwa na Meneja Miradi wa shirika hilo nchini, Bi. Doroth Ndege, aliposoma taarifa ya utekelezaji wa mpango huo kwa Afisa wa Tarafa ya Kisesa, Bw. Fabian Mgina.

Alisema hayo wakati akifungua makambi ya afya kwa shule za msingi wilayani hapa katika Kijiji cha Mwakoluba.

Bi. Ndege alisema kwa kipindi cha mwaka mmoja, shirika lake limetekeleza miradi mitatu ambayo ni kusaidia mtoto shuleni, ufadhili wa watoto yatima na utunzaji wa nafaka katika kijiji cha Mwabusalu.

Alisema malengo ya mpango wa kumsaidia mtoto shuleni, ni kuboresha mazingira ya kujifunzia na huduma za kiafya katika shule za msingi, kuimarisha ushiriki wa wadau mbalimbali na kusogeza huduma za maji kwa watoto shuleni.

Bi. Ndege alisema shirika lake pia limeweza kuhamasisha jamii katika ushiriki wa miradi ya maendeleo kupitia serikali za vijiji na kamati za shule, kwa kujenga vyoo na kutengeneza samani katika shule zote zilizoko kwenye mradi huo.

Alisema hadi sasa madawati 1,600, viti 224, meza 224 na kabati 80, vimetolewa na shirika hilo katika shule 16 za tarafa za Kimali, Kisesa na Nyalanja.

Kutoka gazeti la Nipashe

skip navigations | Japanese (日本語) | Japan Embassy of Japan in Tanzania 在タンザニア日本国大使館 Top Page | About Us | Bilateral Relations|ODA | Visiting Japan |

[Grant Assistance for Grassroots Human Security Projects]

The Signing Ceremony for the Project for Construction of Girls’ Hostel at Meatu Secondary School in Meatu District, Shinyanga Region,

the Project for Construction of Igaga/Itilima Dispensaries in Kishapu District, Shinyanga Region, and the Project for Construction of Homboza Dispensary in Kisarawe District, Coast Region

On 13 November, 2008, the Government of Japan has extended grant aid up to US$ 262,391 (approximately 295 million Tanzanian Shillings) for the following three projects through the scheme of Grant Assistance for Grassroots Human Security Projects (GGHSP). The contracts for the projects were signed between H.E. Mr. Makoto Ito, Ambassador of Japan and the representatives of the respective organizations.

The Project for Construction of Girls’ Hostel at Meatu Secondary School in Meatu District, Shinyanga Region;

a grant worth up to US$ 87,802 (approximately 99 million Tanzanian Shillings) to Meatu District Council for construction of Girls’ hostel at Meatu Secondary School in Meatu District. The project is expected to improve educational environment to benefit 80 girls at the school.

The Project for Construction of Igaga/Itilima Dispensaries in Kishapu District, Shinyanga Region;

a grant worth up to US$ 86,218 (approximately 97 million Tanzanian Shillings) to Kishapu District Council for construction of Igaga/Itilima Dispensaries in Kishapu District. The project is expected to improve health care to benefit about 14,000 residents both in Igaga and Itilima villages, and nearby villages.

The Project for Construction of Homboza Dispensary in Kisarawe District, Coast Region;

a grant worth up to US$ 88,371 (approximately 99 million Tanzanian Shillings) to Lumbesa Group (local NGO) for construction of Honboza Dispensary in Kisarawe District. The project is expected to improve health care to benefit about 40,000 inhabitants in Homboza Village and Msimbu Ward.